Saturday, November 29, 2014

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI YA TIMU YA VIJANA YA COASTAL UNION U-20 MABINGWA WA KOMBE LA UHAI LEO KOROGWE

KATIBU MKUU WA COASTAL UNION KASSIM EL SIAGI AKIZUNGUMZA NA WACHEZAJI WA COASTAL UNION U-20 LEO KABLA YA KUANZA SAFARI KUELEKEA WILAYANI KOROGWE KUCHEZA MECHI YA KIRAFIKI NA KOROGWE UNITED

KIKOSI CHA COASTAL UNION U-20 KILICHOANZA KWENYE MECHI HIYO YA LEO NA KOROGWE UNITED,AMBAPO KABLA YA KUANZA MTANANGE HUO KULINYESHA MVUA KUBWA AMBAYO ILIPELEKEA MCHEZO HUO KUSIMAMA KWA DAKIKA KADHAA KABLA YA KUENDELEA

KUSHOTO NI MKURUGENZI WA UFUNDI WA KOROGWE UNITED,FILBERT MPENZIA AKIMUELEZA KITU MJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI YA COASTAL UNION SALIMU BAWAZIR LEO WA KWANZA KULIA NI NAIBU KADHI MKUU WA TANZANIA,SHEIKH ABUBAKARI ZUBEIR.

KIKOSI CHA COASTAL UNION KIKIPASHA KABLA YA KUANZA MPAMBANO HUO LEO



WALINDA MILANGO WA COASTAL UNION U-20 WAKIPASHA KABLA YA KUANZA MPAMBANO HUO LEO



MKURUGENZI WA BENCHI LA UFUNDI LA COASTAL UNION,MOHAMED KAMPIRA AKISISITIZA JAMBO KWA WACHEZAJI WA TIMU HIYO WAKATI WA MAPUMZIKO KUSHOTO NI MCHEZAJI WA ZAMANI WA COASTAL UNION NA MJUMBE WA KAMATI YA USAJILI RAZACK KAREKA LRO

MASHABIKI WA SOKA WALIOJITOKEZA KWENYE UWANJA WA SOKA CHUO CHA UALIMU KOROGWE WAKIFUATILIA MPAMBANO HUO LICHA YA KUNYESHA MVUA KUBWA

Tuesday, November 25, 2014

COASTAL UNION U-20 YAIKALISHA MONGA STARS YA VYERU WILAYANI MKINGA,YAIPIGA 1-0

KIKOSI CHA U-20 CHA COASTAL UNION KIKIPASHA KABLA YA KUANZA MECHI HIYO DHIDI YA MONGA STARS AMBAPO COASTAL UNION U-20 ILIIBUKA NA USHINDI WA BAO 1-0 BAO HILO LILIFUNGWA NA ZAMIRU ISSA DAKIKA YA 36

MAKIPA YA KIKOSI CHA U-20 COASTAL UNION WAKIPASHA KABLA YA KUANZA MECHI HIYO LEO


KOCHA WA KIKOSI CHA U-20 YA COASTAL UNION,JOSEPH LAZARO AKISISITIZA JAMBO KWA WACHEZAJI WA TIMU HIYO KABLA YA KUANZA MECHI HIYO LEO

KIKOSI CHA COASTAL UNION U-20 AMBACHO KILICHEZA NA MONGA STARS LEO NA KUWAFUNGA BAO 1-0

MWAMUZI WA MECHI HIYO,KASID KITENDO AKIWA NA WACHEZAJI WA TIMU ZOTE MBILI KABLA YA KUANZA MPAMBANO HUO

KIKOSI CHA MONGA STARS KILICHOPIGWA KIMOJA NA COASTAL UNION U-20 LEO

KOCHA WA TIMU YA VIJANA YA COASTAL UNION U-20 JOSEPH LAZARO AKISISITIZA JAMBO KWA WACHEZAJI WA TIMU HIYO LEO WAKATI WA MAPUMZIKO

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA COASTAL UNION,HEMED AURORA WA PILI KUTOKA KULIA AKIFUATILIA MECHI HIYO NA VIONGOZI WENGINE WA TIMU HIYO WA KWANZA KULIA NI MENEJA WA TIMU YA COASTAL UNION AKIDA MACHAI NA KUSHOTO NI MJUMBE WA KAMATI YA USAJILI SALIM BAWAZIRI NA MWANACHAMA WA COASTAL UNION LEO


Wednesday, November 5, 2014

PICHA TANO ZA MENEJA WA COASTAL UNION AKIBADILISHA MAWAZO NA MWENYEKITI WA TANGA MIDDLE VETARAN JUZI.

MENEJA WA COASTAL UNION AKIDA MACHAI AKIBADILISHANA MAWAZO NA MWENYEKITI WA TANGA MIDDLE AGE VETERAN.



HAPA KUSHOTO NI MENEJA WA COASTAL UNION AKIDA MACHAI ALIYESIMAMA AKIZUNGUMZA JAMBO NA MENEJA WA UWANJA WA CCM MKWAKWANI ,MBWANA MSUMARI.



COASTAL UNION :MTAIPENDA MSIMU HUU.

NA OSCAR ASSENGA,TANGA.  

KOCHA MKUU wa Coastal Union ya Tanga, Yusuph Chippo amesema anaamini mipango ya timu hiyo ya kuchukua ubingwa wa Ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu yatatimia na hivyo lazima watanzania lazima wataipenda.
Coastal Union ya Tanga ni timu ambayo imeanza vema msimu mpya wa Ligi kuu soka Tanzania bara ambapo kwa sasa ina pointi 11 ikishika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi kuu.

Alisema kuwa mikakati yake ni kuhakikisha kila mechi timu hiyo inapata matokeo mazuri yatayoiwezesha kufanikisha ndoto zao kufanya mapinduzi kwenye michuano hiyo ambayo inashirikisha timu kumi na nne.

Aidha alibainisha kuwa kikubwa ambacho anajivunia ni kuwa na kikosi madhubuti ambacho kimempa dira ya mafanikio mbeleni yanayotokana na usajili mzuri ambao timu hiyo ilifanya kabla ya kuanza msimu huu.

   “Kwa hakika Coastal Hii lazima mtaipenda sasa tunajiandaa
kuwakabili wanaramaramba tukiwa na lengo moja tu la kupata pointi tatu muhimu ili kuweza kuendeleza rekodi yetu ya ushindi kama ilivyokuwa kawaida yetu “Alisema Chippo.

Akizungumzia mechi hiyo,Chippo alisema kuwa wachezaji wa timu hiyo wanaendelea na mazoezi ya kuhakikisha wanapata pointi tatu muhimu kwa sababu hilo linawezekana kutokana na wachezaji mahiri wanaounda kikosi cha Wagosi hao wakaya.

Coastal Union itaingia kwenye mechi yao na Azam Fc mwishoni mwa wiki ikiwa na kumbukumbu ya kupata matokeo mazuri kwenye mechi yao ambapo iliibuka na ushindi wa mabao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani.