Tuesday, October 21, 2014

COASTAL UNION YAANZA KUIPIGIA HESABU KAGERA SUGAR


TIMU ya Coastal Union ya Tanga imeanza maandalizi ya kuelekea mechi yao na Kagera Sugar itakayopigwa wikiendi hii kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba ikiwa ni muendelezo wa Ligi kuu soka Tanzania bara.
Kauli hiyo ilitolewa na Kocha Mkuu wa Coastal Union,Yusuph Chippo mara baada ya kumalizika mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea kwenye viwanja wa shule ya Sekondari Popatlaly mjini hapa.
Alisema kuwa kikosi chake kipo imara kuweza kuwavaa wakata miwa wa bukoba kutokana na kuimarisha sehemu mbalimbali kwenye timu hiyo hasa mapungufu yaliyojitokeza kwenye mechi yao na Mgambo Shooting ambapo Coastal ilishinda bao 2-0.
Kocha huyo alisema kuwa wembe uliotumika kuwanyoa timu hiyo ya Mgambo Shooting ndio ambao watautumia ili kuweza kupata pointi tatu muhimu wakiwa ugenini lengo likiwa kuweza kuwa kwenye nafasi za juu kwenye msimamo wa Ligi kuu .
“Tunamshukuru mungu kwa kupata pointi tatu muhimu kwenye mechi hii na hili linatokana na kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwenye mechi yetu iliyopita lakini kubwa ni umoja na mshikamano uliopo “Alisema Chippo.

Hata hivyo aliwataka wachezaji wa timu hiyo kuhakikisha wanapambana vilivyo kila mchezo ili waweze kupata matokeo mazuri yatakayowawezesha kuirudishia heshima timu hiyo yenye maskani yake barabara 11 jijini Tanga.
Katika hatua nyengine,Timu hiyo inatarajiwa kutumia usafiri wa ndege kuelekea mkoani Kagera kucheza mechi yake ya Ligi kuu wikiendi hii dhidi ya Kagera Sugar mechi itakayochezwa uwanja wa Kaitaba.

Sunday, October 19, 2014

HIVYO NDIVYO COASTAL UNION ILIVYOWEZA KUCHUKUA POINTI TATU MBELE YA MGAMBO SHOOTING

KIKOSI CHA COASTAL UNION KILICHOILAZA MGAMBO JKT BAO 2-0,

KOCHA MKUU WA COASTAL UNION YUSUPH CHIPPO KUSHOTO NA KOCHA MSAIDIZI BENARD MWALALA WAKIJADILIANA JAMBO WAKATI WA MAPUMZIKO.





WA PILI KUTOKA KUSHOTO NI KATIBU WA COASTAL UNION KASSIM EL SIAGI NA WAJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI SALIM AMIRI NA ALBERT PETER.

WA PILI KUTOKA KULIA NI MENEJA WA COASTAL UNION AKIDA MACHAI NA ANAYEFUATIA NI ALIYEKUWA MWENYEKITI WA COASTAL UNION MZEE HEMED AURORA WAKIFUATILIA MECHI KATI YA M,GAMBO NA COASTAL UNION

WA KWANZA ALIYESIMAMA KUSHOTO NI MENEJA WA COASTAL UNION AKIDA MACHAI AKIZUNGUMZA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA SOKA MKOA WA TANGA TRFA



Thursday, October 9, 2014

COASTAL UNION YAIFUNDISHA SOKA PANONI FC YA KILIMANJARO,YAICHAPA MABAO 2-1,MKWAKWANI.

                      


TIMU ya Coastal Union “Wagosi wa Kaya”jana waliendelea vema na maandalizi ya mechi zake zilizosalia katika michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kuibamiza mabao 2-1 timu ya Panoni FC ya Kilimanjaro mchezo ambao ulichezwa uwanja wa CCM Mkwakwani.


Mchezo huo wa kirafiki ambao ulikuwa na burudani ya aina yake kutokana na timu zote kuonyesha kandanda nzuri na la kuvutia ambapo bao la kwanza la Coastal Union lilifungwa na Keneth Masumbuko dakika ya 23.


Bao hilo lilidumu mpaka timu zote zinakwenda mapumziko ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa timu zote kushambuliana kwa zamu.


Wakionekana kujipanga vilivyo baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake,Coastal Union waliweza kuutawala mchezo huo kwa kipindi hicho huku wakicheza pasi fupifupi na ndefu hali iliyopeleka kuandika bao la pili dakika ya 68 kupitia Omari Mahamudi “Hanzy”


Baada ya bao hilo kuingia langoni mwao, Panoni FC waliweza kubadilika na kucheza kwa umakini mkubwa hali iliyopelekea kupata bao la kufutia machozi kwenye dakika ya 82 kupitia Laurance Mbawa “Tevez”.


Akizungumza mara baada ya kumalizika mchezo huo,Kocha Mkuu wa Coastal Union,Yusuph Chippo aliwapongeza wachezaji wake kwa kupata ushindi lakini akiwasihi kuhakikisha wanakuwa makini kwenye mechi za ligi kuu ikiwemo kucheza kwa hari kubwa ili kuweza kupata pointi tatu muhimu.


Coastal Union inatarajiwa kucheza na Mgambo Shooting zote za jijini Tanga ikiwa ni Daby ya Tanga ambayo inatazamiwa kuwa na upinzani mkubwa kutokana na historia ya timu hizo mbili.

Tuesday, October 7, 2014

HIVI NDIVYO COASTAL UNION ILIVYOWAKALISHA NDANDA SC MKWAKWANI

KIKOSI CHA COASTAL UNION KILICHOICHAPA NDANDA SC MABAO 2-1 UWANJA WA CCM MKWAKWANI JUZI

KOCHA MKUU WA COASTAL UNION YUSUPH CHIPPO AKIWAPA MAELEKEZO WACHEZAJI WAKE.

KOCHA CHIPPO AKITOA MAELEKEZO KWA MSHAMBULIAJI WA COASTAL UNION RAMA SALUMU NAMNA YA KWENDA KUHAKIKISHA TIMU INAPATA USHINDI KWENYE MECHI YAO YA LIGI KUU DHIDI YA NDANDA SC ILIYOMALIZIKA KWA COASTAL UNION KUIBUKA NA USHINDI WA MABAO 2-1.

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA COASTAL UNION HEMED AURORA AKIWA NA MAHUNDI KWENYE MECHI HIYO

KUSHOTO NI KOCHA CHIPPO KATIKATI NI ALIYEKUWA MWENYEKITI WA COASTAL UNION HEMED AURORA ANAYEFUATIA NI MKURUGENZI WA UFUNDI MOHAMED KAMPIRA NA MJUMBE WA KAMATI YA USAJILI RAZACK KHALFANI "KAREKA: WAKIJADILI JAMBO

MBUNGE WA JIMBO LA TANGA,OMARI NUNDU KUSHOTO AKISAMILIMIANA NA ALIYEKUWA MWENYEKITI WA COASTAL UNION HEMED AURORA KABLA YA KUANZA MCHEZO WA LIGI KUU SOKA TANZANIA BARA JUZI KATI YA NDANDA SC NA COASTAL UNION

KATIKATI NI ALIYEKUWA MWENYEKITI WA COASTAL UNION HEMED AURORA,KUSHOTO KWAKE NI KOCHA MSAIDIZI WA COASTAL UNION BENARD MWALALA,KULIA NI KOCHA MKUU YUSUPH CHIPPO WAKIWA KATIKA MAZUNGUMZO



WA KWANZA KULIA NI MAKAMU MWENYEKITI WA COASTAL UNION STEVEN MGUTO AKIWA NA WANACHAMA WA TIMU HIYO AKISHUHUDIA MECHI KATI YA NDANDA SC NA COASTAL UNION JUZI

KOCHA MKUU WA COASTAL UNION YUSUPH CHIPPO AKIMPA MAELEKEZO MSHAMBULIAJI WA TIMU HIYO RAMA SALUM KABLA YA KUINGIA UWANJANI JUZI

BAADA YA USHINDI MASHABIKI NAO HAWAKUWA NYUMA KUSHANGILIA

WA KWANZA KUSHOTO NI MHASIBU WA COASTAL UNION KAKERE AKIFUATIWA NA MNEC WA WILAYA YA MKINGA,OMARI MWASINGO NA MNEC WA WILAYA YA PANGANI JUMAA WAKIFUATILIA MECHI HIYO