Sunday, September 14, 2014

COASTAL UNION YALAZIMISHWA SARE NA MTIBWA SUGAR ZATOKA 1-1.

                         

TIMU ya soka Coastal Union ya Tanga leo imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Mtibwa Sugar ya Morogoro ikiwa ni mechi ya kirafiki kuelekea maandalizi ya msimu mpya wa Ligi kuu Tanzania bara mchezo uliopigwa uwanja wa CCM Mkwakwani.

Katika mchezo ambao ulikuwa mkali na wenye upinzani mkubwa kutokana na timu zote kushambuliana kwa zamu na kuonyesha kandanda nzuri na la kuvutia, Mtibwa Sugar ndio ilikuwa ya kwanza kuweza kupata bao lake lilikfungwa na Mussa Nampaka dakika ya 44.

Bao hilo lilidumu mpaka timu zote zinakwenda mapumziko ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kila timu iliweza kuingia uwanjani hapo zikiwa na hari mpya baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake.
Wakionekana kujipanga vilivyo kwenye awamu hiyo ya lala salama,Coastal Union walianza kufanya mashambulizi ya kushtukiza langoni mwa Mtibwa Sugar kwa dakika kadhaa hali iliyopeleka kupatikana bao la kusawadhisha lililofungwa na Itubu Imbem Guelor.

Baada ya kumalizika mchezo huo, Kocha Msaidizi wa Coastal Union,Benard Mwalala alisema mchezo huo ni kipimo tosha kwa timu hiyo kuangalia sehemu gani yenye mapungufu kabla ya kuvaana na Simba kwenye mechi ya ufunguzi wa Ligi kuu.

  “Ninachoweza kusema mapungufu yaliyojitokeza kwenye mechi hii tutayafanyia kazi kwa asilimia kubwa lengo likuwa kuhakikisha tunapata matokea mazuri kwenye mechi zetu za ligi kuu “Alisema Mwalala.
Coastal Union:Gk Shabani Kado,Razack Khalifani,Hamadi Juma,Mbwana Kibacha,Yayo Kato Lutimba,Itubu Imbem Guelor,Bakari Mtama,Ramadhani Salum,Sbri Twaha,Abdallah Mfuko,Aypub Semtawa.
Kwa upande wa Mtibwa Sugar:Saidi Mohamed,Hassani Ramadhani,David Luhende,Andrew Vicent,Salim Mbonde,Shabani Nditi,Ally Shomari, Mzamiru Yassin,Ame Ally,Mussa Mgosi na Mussa Nampaka.
Coastal Union walifanya mabadiliko kwa kuwatoa Hamadi Juma,Razack Khalfani,Yayo Lutimba na Ayoub Semtawa na kuwaingiza Amani Juma,Tumba Sued,Petro Mahundi,Obina Bright na Hussein Sued.
Nao ka upande wao,Mtibwa Sugar walifanya mabadiliko kwa kuwatoa Mussa Nampaka,Mzamiru Yassin,Amme Ally na kuwaingiza Mohamed Mkopi,Hassani Mbande na Mohamed Ally.

No comments:

Post a Comment