Friday, September 26, 2014

CHIPPO AWEKA MIPANGO YA KUCHUKUA POINTI TATU DHIDI YA MBEYA CITY KESHO SOKOINE.

 
KOCHA MKUU wa Coastal Union ya Tanga,Yusuph Chippo amesema kuwa malengo yake makubwa ni kuhakikisha timu hiyo inapata ushindi dhidi ya Mbeye City mchezo unaochezwa kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Akizungumza leo ,Kocha Chippo alisema kuwa kuelekea mechi hiyo hakuna hata mchezaji mmoja ambaye ni majeruhi hivyo wana uhakika wa kuhakikisha wanapata matokea mauziri kwenye mechi hiyo.
Coastal Union iliwasilia mkoani Mbeya juzi ambapo jana ilifanya mazoezi yake kwenye uwanja wa soka Polisi na uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya ikiwa kwenye maandalizi ya mwisho kabla ya kuvaana na wapinzani wao hao.

  “Sisi tunapambana kuhakikisha matokeo mazuri yanapatikana kwa sababu hilo ndilo lengo letu kuu hii inatokana na usajili wa nguvu tulioufanya msimu huu na umakini wa wachezaji tuliokuwa nao “Alisema Chippo.
Coastal Union itavaana na Mbeya City kesho(leo) kwenye uwanja huo ikiwa ni muendelezo wa Ligi kuu soka Tanzania bara ambapo mchezo wa kwanza ilicheza na Simba SC kwenye uwanja wa Taifa na kutoka sare ya kufungana mabao 2-2.


Kwa upande wake,Kocha wa makipa,Razack Siwa amesema kwenye idara yake ya walinda milango ipo imara kuhakikisha wanakuwa imara kwenye mechi hiyo.

No comments:

Post a Comment